Tuesday, November 29, 2016

Vanessa Mdee ndani ya MTV Shuga (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Baada ya watu kibao kujitokeza kufanya audition ili kushiriki katika tamthilia ambayo imejishindia tuzo , Vanessa Mdee ametajwa kama moja ya washiriki ambao watahusika katika tamthilia hiyo ya Shuga sehemu ya tano.
MTV Shugar ni tamthilia ambayo inaelezea mapenzi, muziki, mahusiano na Drama ambavyo vyote hivi ni moja ya issue ambazo zinawazunguka watu katika maisha yao ya kila siku, baada ya season nne kufanyika Kenya na Nigeria, inakuja tena kwa mara nyingine South Afrika  kama sehemu ya 5 huku ikiongozana na Vanessa Mdee, Thuso Mbedu, Mohau Mokoatle Cele, Jezriel SkeiEmmanuel Ifeanyi, Nick Mutuma na Adesua Etomi wakiwa na crew nzima ya MTV Shuga.

Hanscana afunguka kuhusu wasanii wa bongo kurudia na kufanana kwa video zao (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Muongozaji wa video na mshindi wa Tuzo za Watu 2015, Hanscana ambae pia ametisha sana kwenye utengenezaji wa video mpya ‘Muziki’ ya Darasa, pia ndiye director anayekuja kwa kasi kutokana na ubora wa kazi zake.
Muongozaji huyo na mtayarishaji wa video nchini Hanscana, amesema sababu inayo pelekea video nyingi za bongo kurudiwa na kufanana ni kutokana na maamuzi na mapendekezo ya msanii mwenyewe anacho pendelea.
Hanscana
Akipiga story ndani ya eNewz amesema “Ukiona kuna kitu kimerudiwa katika video ujue kuna makubaliano kati ya muongozaji na msanii kwa kuwa mara nyingi msanii anapo andika wimbo wake anakuwa na wazo la aina ya video ambayo anaitaka hivyo wasanii ni kama wateja wetu na tunafanya anachokitaka mteja wetu”.
Pia Hanscana amesema kwamba yeye na Khalfani ni marafiki japo hawajawahi kufungua kampuni moja ila wakati wanatafuta maisha waliwahi kuishi nyumba moja kwa sasa kinacho watenganisha ni kutokana na kila mmoja kuzidi kutafuta maisha yake japo bado ni marafiki.

album mpya ya Navy Kenzo “AIM” (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Ebhana AIM ndio album ya kwanza ya Afro pop ambayo inategemewa kutoka mwaka huu mwezi Disemba, na hii ikiwa katika kipindi ambacho wasanii wengi na record label hawaamini juu ya album kutokana na wasambazaji kuwa wachache.
Akiongea na Perfect255, muhudumu wa mauzo ya Album ya AIM, amefunguka na kusema kwamba kwa sasa wanapokea pre order ila pia wameweka katika vituo mbalimali ambavyo vitakuwa ni kuponi ambazo zinakodi, kwahiyo mtu akitoa order yake anapatiwa koponi yake.
“Kwa sasa tunachukua pre order, lakini tumeweka pia kwenye vituo mbalimbali ambazo sisi tumeweka kitu kinaitwa kuponi, kuponi hizo zinakuwa na kodi ambazo mtu akitoa order yake anapewa hiyo kuponi, tumefanya syteam ambayo inaitwa pre order ili iweze kumfikia kila mtu, nikimaanisha kwamba Pre order unaweza kulipia hata nusu, hata robo kwamba ninauwakika nitaichukua hii album, yaani unaweza kulipa kwa vibubu mpaka pale utakapomaliza order yako…….Usambazi tutafanya wenyewe kama wenyewe, Album ikishatoka bei nayo itaongezeka na ndio maana tumeweka pre order, kwahiyo ile namba ambayo tumeweka pale mtu ndio atatumia kununua kutuma pesa yake, picha yake kama akitaka tumposti na akaunti yake ya Instagram….mpaka sasa tumepata sapoti kubwa ambayo kila msanii amekuwa akinunua kuonyesha love..na wasanii wengine ambao watakuwepo kwenye album yetu pia tutawatangaza kupitia XXL.”
Album ya AIM unaweza kupreorder kwa gharama ya 10,000tzs na unaweza kutoa oda yako kwa kutumia namba ya simu ya +255656762983 ili kuenjoy album yako ya AIM.

KESHO WATASEMA NI LEVEL ZINGINE (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

RUDE ZONE MUSIC PRESENTS #KESHO_WATASEMA official single
Bofya hapa https://mkito.com/song/14424 kupakua na kusikiliza KESHO WATASEMA ya kwake Rude Rodgers Babalao @rodgersbabalao27 Contact +255756978662
Produced by GS @gssehaba & FEX
#InfoPoweredBy @babalaotv @rodgersbabalao27 www.babalaoinc.blogspot.com Cc. @djmwanga @prosper_prior @adammchovu @gnakowarawara @juma_jux @johmakinitz @nikkwapili @jabirsaleh @mamybabie @annapetertz @chaba009 @djchoka @defxtro @jaymoe @jcbmakalla @bdozen @africanmusicnow @chindomanwatengwa @daznaledge @director_tonnytrigger @akimurobby1 @kyomushula @mtublack_2016 @djnoel255

Friday, November 25, 2016

Ben Pol-: Mimi sihitaji KIKI ili muziki wangu upenye (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Ni kwenye Clouds E ya Clouds TV na Shadee Weriss ambapo Ben Pol alikuwa na interview kuzungumzia muziki mpya ambao ameshirikishwa na Darassa unaoitwa Muziki.
Ben Pol amefunguka kuwa kwa kipindi hiki ambacho ni ngoma kibao zimetoka kwa mkupuo itachukua takriban wiki 3 ili ngoma hizo kujichuja na muziki mzuri kuendelea kuishi muda mrefu zaidi ya hapo  na zingine ambazo zimetoka kwa kiki kuishia hewani.
“Sisi hatuhitaji kiki ili muziki wetu kupenya, siku zote muziki ambao unatoka kwa kiki sio muziki mzuri, inadhihirisha kuwa muziki huo haujitoshelezi ndio maana unatafutiwa kiki ili kuupa nguvu.” Alisema Ben Pol.
Tangu wiki hii imeanza ni zaidi ya ngoma 5 zimeshaachiwa ikiwa ni pamoja na Dume Suruali ya Mwana FA na Vanessa Mdee, Nitampigia ya Stamina na Mr Blue, Kokoro ya Rich Mavoko na Diamond, Muziki ya Darassa na Ben Pol pamoja na  Mwendo Tu wa Songa na Jay Moe.

Mwana Fa: Vita za kimuziki ni sehemu ya kukuza kazi ya Sanaa(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Vita ya Diamond na Ommy Dimpoz ni moja ya vita ambayo imefanya mashabiki wengi kuwa na maswali , ila kwa upande wa Mwana Fa yeye anajibu moja tu kwamba upinzani ni sehemu ya kukuza kazi ya sanaa.
Baada ya kuachia Dume Suruali ambayo inatarajiwa kufanya vizuri kwenye chart za Bongo mpaka nje ya nchi, Mwana Fa ameamua kufunguka juu ya vita ambayo imeibuka kati ya Ommy Dimpoz pamoja na Diamond.
Mwana Fa aliamua kufunguka na kusema kwamba mambo ya vita kati ya wasanii wetu hatujaanza kuyaona kwenye muziki wetu peke yake, ishu kama ya Siasa, Mpira hata vyombo vya radio vyote hivi vimekuwa vikikutana na vita ambazo wao kama wao zinakuwa zinawaongezea manufaa kiuchumi.
Upinzani na vita ni moja ya mambo ambayo kwa asilimia fulani yanaweza kukuza kazi ya sanaa, kwasababu hapo ndipo juhudi zinapatikana kwa wasanii wetu ilikuongeza waweze kukua kimuziki.

Thursday, November 17, 2016

Remy Ma asema haya kuhusu beef na wasanii wa kike, collabo na Nicki Minaj na Foxy Brown(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Baada ya kushika chati na album ya pamoja na rapa Fat Joe, Remy Ma ambaye tayari kushatoka kama solo artist na ngoma zake mbali mbali.
Remy Ma
Kwenye mahojiano wiki hii rapa Remy Ma aliyesikika sana kupitia wimbo wa “All The Way Up” na Fat Joe, amesema hapakuwa na kazi iliyo fanyika kati yake na Nicki Minaj.
Remy anasema “Nilipotoka jela Minaj alinipigia simu na tukapanga colabo ila alisema iwe siri na baadae yeye ndio akaivujisha hio siri, kama alitaka wimbo na Foxy Brown angefanya mapema hata bila mimi, watu wanajua tuna vipaji na wanataka kuona vikiwa pamoja ila kwenye maongezi yetu nili muambia kuwa watu wata tugombanisha na ndio kinachotokea sasa ila sina dhima ya kumdiss mtu bila sababu”
Wiki mbili zilizopita Nicki Minaj alisema kuna collabo kati yake na Remy Ma na imetayarishwa na Diplo.
Remy pia anasema ni muda wasanii wa kike waache majigambo yao ili tufanye kazi pamoja kama wakina Drake, Rick Ross, na French Montana wakifanya colabo inakuwa kubwa sana.

Mayweather ndani ya upromota (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Baada ya kufanya kimyakimya kazi ya upromota, sasa bondia nyota Floyd Mayweather ameamua kufanya hadharani. Sasa ameonekana akisimamia pambano la mabondia Badou Jack  (kushoto) na James DeGale (kulia) akiwa ni promota

Sunday, November 13, 2016

Beyonce, Jay Z waangukia kwa Michelle Obama na kumtaka afanye hivi(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Baada ya Hillary Clinton kushindwa katika
uchaguzi mkuu nchini Marekani dhidi ya Donald Trump, nyota wa muziki nchini humo, Jay Z na mke wake, Beyonce, wamemtaka mke wa Barack Obama, Michelle Obama, awanie kiti hicho 2020.
Jay Z na Beyonce
Wasanii hao walikuwa wanamsapoti Hillary katika uchaguzi huo na walikuwa wanaungana baadhi ya sehemu kwa ajili kumnadi, lakini hajafanikiwa kushinda, hivyo wawili hao wameamua kuangukia
kwa mke wa Obama, Michelle, kuwa awanie nafasi hiyo mwaka 2020 wataungana pamoja kwenye kampeni.
Michelle na mume wake, Obama, ni miongoni mwa watu ambao walikuwa wanampigia debe Hillary, lakini hawakufanikiwa.
Novemba 7 mwaka huu, Jay Z aliachia wimbo
mpya ambapo ndani yake kuna mistari inasema kuwa anataka mtoto wake akue huku akiwa anaongozwa na rais mwanamke na hivyo walitamani kuona Hillary kupata nafasi hiyo.
“Nilitamani kuona mtoto wangu akiwa anakua chini ya rais mwanamke, Hillary hajapata nafasi hiyo, lakini ninaamini bado kuna nafasi nyingine
baada ya miaka minne ijayo, nimekuwa nikiongea na Michelle mara kwa mara na ninaamini atafanya hivyo,”
alisema Jay Z.

Muongeze Young Dee kwenye List ya watu hawa!(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Hitmaker wa ngoma ya “Hands Up” Young Dee ameendelea kuongeza list ya mastaa kutoka Bongo Flevani wenye followers wengi zaidi katika mtandao wa instagram.
Ni baada ya kutimiza followers Million 1 katika mtandao wa instagram na kuongeza idadi ya mastaa kutoka  Tanzania wenye followers wengi zaidi katika mtandao huo.
Mastaa wengine wakubwa duniani ambao wametimiza followers Million 1 hivi karibuni ni pamoja na Fat Joe hit maker wa ngoma ya “All the way up” wa nchini Marekani.

Hatimaye Series ya mauaji ya 2 Pac na BIG kutua kwenye TV(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Wakati mashabiki wanasubiri filamu ya maisha ya Tupac, All Eyez On Me itoke, USA Networks, imetangaza kuwa itaachia drama ya uhalifu wa
kweli kuhusu mauaji ya Pac na The Notorious B.I.G.
Vifo vya Shakur na Biggie vimewahi kuandikwa kwenye vitabu vingi na documentaries kadhaa.
2 PAC & B.I.G
Series hiyo itajulikana kwa jina la Unsolved, The Hollywood Reporter imeripoti kuwa series hiyo
itatoka ndani ya miezi 12 ijayo.
Series hiyo itajikita kwenye kazi ya mpelelezi wa LAPD Detective Greg Kading, aliyeongoza uchunguzi wa mauaji hayo.
Mpelelezi huyo alishawahi kuandika pia kitabu kiitwacho Murder Rap: The Untold Story of Biggie Smalls & Tupac Shakur. Murder Investigations, ambayo ilifanyiwa documentary yenye jina hilo pia.

Friday, November 11, 2016

Alichoandika Alikiba baada ya kutangazwa mshindi halali wa tuzo ya MTV EMA Best African Act(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Imetangazwa rasmi na waandaaji wa tuzo hizo za MTV EMA kuwa Alikiba ndiye mshindi halali wa tuzo ya MTV EMA category ya Best African Act.
Kupitia kurasa yake ya instagram Alikiba ameamua kuchukua nafasi ya kuwashukura watu wake wa karibu pamoja na mashabiki zake kwa sapoti ambayo wanampa hadi kuhakikisha ameipata tuzo hiyo.Namshukuru MUNGU Na Shukrani kwa MTV kwa heshima hii, nina furaha sana kwa ushindi huu, ni heshima kwangu na nchi yangu Tanzania 🇹🇿 pamoja na East Africa nzima kiujumla. Shukrani sana kwa familia yangu, management yangu na mashabiki zangu wote.
 Ningependa pia kuchukua nafasi hii kushukuru vyombo vya habari vyote, watangazaji, waandishi na wadau wote wa sanaa kiujumla kwa kunisapoti katika kazi zangu. Lastly, nawashukuru wasanii wenzangu wote mlionipa ushirikiano na kuthamini kipaji changu kwa kuniombea kura zilizonipa ushindi. Ushindi wangu ni ushindi wa sanaa yetu sote. Proudly Tanzanian 🇹🇿 MUNGU awabariki sana. #TupoPamoja #Kajiandae #KingKiba

Issue ya Wizkid na Alikiba, Jux awachana MTV kwa kuwafanyia figisu Watanzania kwenye tuzo zao(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Ushindi wa tuzo ya Alikiba kwenye tuzo za MTV EMA ambayo awali alipewa Wizkid umefichua mambo mengi kiasi cha kuanza kuwapa wasiwasi wasanii wa Tanzania.
Jux ameamua kufunguka ya moyoni kwa waandaji wa tuzo hizo, huku akiwalaumu kwa kuacha watu wapige kura huku washindi wanawapendekeza bila ya hata kuzingatia kura za mashabiki. Jux anaamini kama zoezi la upigaji kura kwenye MTV EMA lisingekuwa wazi Alikiba asingeshinda tuzo ambayo anastahili.
Jux pia amesema polls za upigaji kura kwenye tuzo za MAMA’s nzo zingekuwa wazi basi tuzo hizo zingerudi nyumbani, amedai kuwa anaamini Diamond alishinda lakini walimpa Wizkid.

Fid Q: Zama za wana Hip hop kufanya video rahisi zimepita (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Fid Q amesema zama za wasanii wa hip hop kufanya video rahisi umepitwa na wakati na kwamba wasanii sasa wanatakiwa kuumiza vichwa zaidi.
 Fid Q
Amedai kuwa mashabiki wa sasa wanataka kuona video ambayo inaweza kuwavutia machoni.
“Ni muda mrefu sana wasanii wa hip hop wamekuwa wakifanya video simple tu, ndio hip hop is the realness of reality lakini tunaishi katika zama ambazo biashara imetoka kwenye showbiz inaenda mpaka kwenye eye-candish – ni kwamba watu wanataka waangalie kitu ambacho macho yao yatavutiwa, yapata ladha fulani,” alisema Fid
Hivi karibuni Fid Q ameonesha kulizingatia hili kwa kutoa video zenye viwango tofauti na zile alizokuwa akizitoa mwanzo.

Yemi Alade anyoosha maelezo na kutoa sababu ya kwanini hana matumizi makubwa kama Davido(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Baada ya Kutajwa kuwa malkia wa Afrobeats na Jarida maarufu nchini Marekani la Fader Magazine, Msanii maarufu kutoka Nigeria huenda pia akawa ni moja ya mastaa ambao ni nadra sana kuwaona wakiposti kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii picha wakila Bata.
Kama tulivyowazoea mastaa wengi wa Afrika na hata wale wasanii wakubwa nchini marekani.
Yemi Alade na Davido
Hii tofauti kabisa kwa mshindi wa tuzo lukuki za kimataifa Yemi Alade, kwani wiki hii wakati ana’cover jarida la fader Magazine aliulizwa swali ni kwa nini hatumii Pesa kama Davido au kama mastaa wenzake wakubwa wa Nigeria?
Yemi Alade alianza kwa kusema “Kwa mtu ambae hujatoka kwenye familia ya kitajiri kama Davido ni ngumu sana kufikia malengo yako” Yemi Alade alianza kwa kusimulia historia yake ya maisha.
“Oooohhh natakiwa nitafute zaidi kwani kuna tofauti kubwa sana kati ya Yemi Alade na Davido, Utakuwa hujakosea ukimuita Davido ni Mtoto wa Kitajiri.” Yemi Alade aliendelea kusema.
“Kwa upande wangu ni Tofauti kabisa, Historia zetu za maisha zinatofautiana kabisa hivyo ni lazima tutofautiane kwenye matumizi. Yeye (Davido) lazima atafute Gari lenye thamani kubwa zaidi Duniani lakini mimi natafuta gari lolote lile ilimradi linifikishe safari.“ Aliendelea, na alizidi kwenda mbali zaidi kwa kusema.
Kabla ya Baba yangu kufariki siku moja aliniletea Bakuli ambalo lilikuwa na maharage ambayo yalikuwa yamechanganyika changanyika na kisha kuniambia unaona nini humu kwenye bakuli..? nikamjibu naona mchanganyiko wa maharage ambayo yamepondeka pondeka na mengine hayajapondeka kabisa. Basi akachukua lile bakuli akaanza kulitikisa baada ya muda akanionesha tena akaniambia unaona nini…?nikamjibu naona mchuzi mzito juu ya bakuli, Basi akaniambia ili ufanane na wao lazima utumie nguvu, Nikanoti hiyo kauli hadi leo hii.”
Yemi Alade alikuwa nchini Marekani wiki hii aki’cover stori kwenye Jarida la Fader Magazine baada ya kutangazwa kuwa ni Malkia wa Afrobeats kwa mwaka 2016.

Nikki Mbishi awajia juu Roma na Tongwe Records, adai Roma kaiba mistari yake kwenye ngoma hii(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Rapa kutoka kundi la Tamaduni Muzik Nikki Mbishi leo kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii ametoa ya moyoni na kudai ya kwamba rapa mwenzake Roma mkatoliki kutoka Tongwe Records ametumia mashairi ya wimbo wake kwenye Cypher
ya Fiesta 2016.
Nikki Mbishi aliandika kwa kuanza kulaumu studio za Tongwe Records kwa kuchelewesha kutoa ngoma zake kwani ndiyo chanzo cha mashairi yake kuibiwa na Roma.
Nikki Mbishi
“Tongwe Records Bwana tunarekodi mangoma makali hawayatoi yapo tu ndani, matokeo yake Roma anachukua Verses za watu anachana yeye!“ aliandika Nikki Mbishi kwenye ukurasa wake wa Twitter.
Aliongeza pia kwa kuandika
“Baada ya kuchana verse yangu kwa jina lake, akarusha na label, so pengine Biggie kamkaribisha Diddy na bad boy”
Hata hivyo Tongwe Records wamemshauri Nikki Mbishi kukaa pamoja na Roma badala ya kuendelea kuchafua Brand yao ya Tongwe Records, kwani wizi huo sio wa Tongwe Records.
Roma nae mpaka sasa hivi hajajibu chochote kuhusu tuhuma hizo za wizi wa mistari.

Tuesday, November 8, 2016

Alichokisema Alikiba baada ya kudai kudhulumiwa kwenye tuzo za MTV EMA(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Ni juzi ndiyo siku ambayo zilikuwa zikitolewa tuzo za MTV Europe Music Awards (MTV EMA) ambapo bendera ya Tanzania ilikuwa ikipeperushwa na mkali Alikiba pande hizo.
Ni Best African Act ndio category ambayo mtu mzima kiba alikuwa akigombania pamoja na mastaa wengine wakubwa Africa akiwemo Wizkid wa Nigeria ambaye ndiye aliye tangazwa kama mshindi wa category hiyo.
Kitu ambacho kimezua utata ni baada ya kura kuonyesha dhahiri kuwa Alikiba ndiye mshindi halali wa tuzo hiyo na kama ilivyokuwa katika categories zingine kuwa mwenye kura nyingi ndiye anapewa tuzo lakini kwenye category hiyo ushindi alipewa Wizkid ikiwa kura aliongoza msanii Alikiba.
Imewagusa wengi wapenzi wa muziki mzuri na kuwaweka katika hali ya sintofahamu kutokana na kitendo hicho.
  Jana Alikiba alikuwepo katika kipindi cha Jahazi cha Clouds FM, na moja kati ya maswali ambayo aliulizwa mkali huyo ni pamoja na hilo la kuhusu MTV EMA.

Idris Sultan -: Natamani Lulu anizalie(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Mshindi wa Big Brother mwaka 2014 Idris Sultan amemtaja mrembo wa Bongo Movie Elizabeth Michael maarufu kama Lulu kuwa ndiye msichana ambaye anaishi katika ndoto zake kwasasa.
“Me naona Elizabeth Michael ametulia sana, ni staa ambaye namuona yuko vizuri, amesimama, mwenye vigezo vya mwanamke ambaye ametulia, anajiheshimu na vitu kama hivyo.”
Hayo ni baadhi tu ya maneno ambayo Idris Sultan alifunguka baada ya kuulizwa ni mrembo wa Bongo Movie ambaye anamtamani kutoka nae.

Wale asakwa na polisi(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Rapper Wale amefunguliwa mashitaka na kampuni ya kuandaa matamasha baada ya kulipwa mtonyo wa dola $25,000 alafu hakutokea jukwaani.
Kupitia mtandao wa Tmz umeripoti kwamba rapper Wale amefunguliwa mashitaka na kampuni ya Upfront and Personal Global kwa kutotokea katika tamasha ambalo alipaswa kuperfome baada ya kupewa $25,000 ikiwa kama mkataba wao waliokubaliana.
Hata hivyo Promoter wa Tamasha hilo amefunguka kwamba walijaribu kumpigia simu Wale lakini alikuwa hapokei, promoter huyo anasema kwamba lengo kubwa la kumtafuta ni kutaka kurudishiwa pesa yao.

Country Boy asema hawezi kufanya ‘Playback’, pia afunguka kuhusu tour yake ‘Dakika 45’ za Country Boy(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Rapa Country Boy amefunguka na kusema kuwa kwa sasa amekua kisanaa hivyo hayuko tayari kufanya ‘Playback’ katika show zake na kwamba sasa anafanya muziki ‘live’ na band yake na ameamua kufanya hivyo kuwaonesha watu kuwa ana uwezo wa kufanya hivyo.
Country Boy
Rapa Country Boy alisema hayo kupitia kipindi cha Bongo Fleva Top 20 ya East Africa Radio na kudai kuwa muziki wake sasa ni mkubwa hivyo haoni sababu ya kuendelea kufanya ‘Playback’ katika show hivyo sasa ni mwendo wa live music pamoja
na band yake.
Pia Country Boy amedai kuwa kwa sasa amenzisha ‘tour’ yake mwenyewe kuzunguka nchi nzima ambayo ameipa jina la ‘Dakika 45’ za Country Boy.
“Sasa hivi nimeanza tour yangu ya ‘Dakika 45’ za Country Boy nafanya live Music, live band, na watu wa Band nyuma, wapiga gitaa, wapiga Solo, Piano, watu wa Drums, kila mtu anafanya set up ya live show.
Aliendelea “hivyo kila nitakapokuwepo nitafanya live show na Band, ni kitu ambacho nataka nikifanye.
Hata ukiangalia wasanii wa Marekani
wanapofanya show wanafanya live mzee, mimi siwezi kufanya ‘playback’ wakati mimi ni msanii mkubwa ambaye nina uwezo wa kufanya vitu kibao.
Nataka kuwa prove watu kuwa nina uwezo
wa kufanya live lakini pia nataka kuwaonyesha energy ndiyo maana nimeweka dakika 45 za Country Boy sidhani kama kuna msanii yeyote anaweza kufanya show ya dakika 45 non-stop ya ngoma zake mwenyewe bila mtu mwingine mimi nimeamua kufanya hivyo”
alimalizia Country Boy

Jokate: Alikiba nakufananisha na Beyonce kimuziki(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Mwanamitindo maarufu Jokate Mwegelo
amefunguka ya moyoni na kumwaga sifa za
kutosha kwa mwanamuziki Alikiba kutokana na uwezo wake kisanaa na namna anavyoendesha maisha yake.
Alikiba
Jokate amesema kuwa kimuziki anaweza
kumfananisha Alikiba na msanii Beyonce kwani ana uwezo mzuri wa kuimba live kwa sauti nzuri, kucheza, kurap na kucheza na mashabiki pindi awapo stejini.
Jokate alimwaga sifa hizo kupitia mtandao wake wa Instagram na kuwataka mashabiki wa Alikiba kumlazimisha msanii huyo aweze kufanya ‘tour’ yake mwenyewe nchi nzima ili aweze kuwafikia mashabiki wengi zaidi ambao wana kiu ya kupata burudani kutoka kwake.
jokatemwegelo-20161027-0002 
Jokate
Ujumbe ulisomeka hivi “Naomba kusema tu wewe hushindani na yoyote hapa Tanzania, kuanzia ladha yako ya muziki unaotengeneza mpaka sauti yako, tena huko kwenye sauti naomba nisiongee maana sitaki upasuke bichwa lako lol ila kuna kitu cha kipekee kwenye sauti yako, you are “The Voice”. Kila siku unakuwa bora zaidi yaani labda nikufananishe na Beyonce kimuziki, usiniue lakini. Ukitaka you can dance, you can sing tena live sauti clear haina mikwaruzo, you can rap, unaweza igiza uchizi yaani you are just perfect kama mwanamuziki. Kama hujui leo ujue. Nakuombea siku moja dunia nzima iweze kufurahia hiki kipaji adhimu kutoka kwako” aliandika Jokate

Friday, November 4, 2016

Diamond Platnumz: Mavoko ana mabomu ya hatari(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Msanii Diamond Platnumz amefunguka na kusema kuwa ukimya wa Rich Mavoko unatokana na msanii huyo kujipanga na kazi zake mwenyewe na kudai mpaka sasa amefanya kazi nyingi na kali sana.
Rich Mavoko
Diamond Platnumz alisema hayo hivi karibuni kupitia kipindi cha Friday Night Live na kusema kuwa Rich Mavoko amefanya kazi nyingi lakini yeye mwenyewe anaziweka pembeni na kutaka kufanya kazi kali zaidi.
“Mimi mwenyewe nimefanya nyimbo nafikiri mbili na Richard na muda wowote zinaweza kutoka, sema Richard ni mtu fulani ambaye anajipanga hivyo kipindi hiki anajipanga akianza kufumuka na mabomu yake ni hatari, maana anajipanga kila wimbo akirekodi anakwambia hii bado.
aliendelea “Akirekodi nyingine tena anakwambia hii bado yaani naweza kusema Richard ni msanii ambaye ana nyimbo nyingi sana kali. Kuna wimbo pale unaitwa ‘Sijaona’ WCB nzima wanaikubali lakini yeye anakwambia hii bado, ila akisema hivyo akileta ngoma nyingine inakuwa kali zaidi. Kwa hiyo ni mtu ambaye Mwenyezi Mungu kamjalia kipaji na mwenyewe anakuaga hana papara” alimalizia Diamond Platnumz

Alikiba-: Hakiwezi kunikuta kilichomkuta Davido Sony Music(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Yapata miezi miwili sasa tangu tuzisikie taarifa za msanii mkali kutoka Nigeria Davido kutoa malalamiko kwa uongozi wa lebo ambayo inasimamia kazi zake kwasasa Sony Music.
Malalamiko hayo yalitokana na kilichosemekana kuwa uongozi huo unamzuia msanii Davido kuachia kazi mpya bila kujali kuwa ni kipindi kirefu kimepita kwa msanii huyo bila kutoa kazi mpya.
Kutoka Bongo Flevani msanii Alikiba naye pia yupo chini ya uongozi huo wa Sony Music. Ila yeye amesema kuwa jambo kama lile lililomtokea Davido yeye haliwezi kumkuta kutokana na mkataba wake ambao amesaini na kampuni hiyo.
Ni baada ya kuulizwa kuwa yeye amejipanga vipi kama endapo litatokea kama lililomtokea msanii mwenzake Davido katika lebo hiyo.
“Nimejiandaa vizuri, na pindi unapokuwa unasaini kitu ina maana kuwa umekubaliana na kila kitu, kwahiyo mimi pia nina matakwa yangu na hata wao pia wana matakwa yao, kwahiyo kitu ambacho kipo hapo ni kwenda na agreement. Me siwezi kukaa muda zaidi ya miezi 3 bila kutoa ngoma, na huo ndio mkataba wangu jinsi unavyosema.”

Joh Makini awachana wanaoanzisha ‘lebo’(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Rapa mkali kutoka Weusi Joh Makini amewachana wanaoanzisha label hapa nchini kuwa wengi wao hawajui vigezo vya kumiliki label na badala yake wanazitumia label kama kiki katika muziki wao.
Joh Makini
Akipiga story ndani ya eNewz amesema, Weusi wana mipango mingi ikiwemo kuanzisha label yao japo wana baadhi ya vijana wanaowasaidia lakini hawa wezi kujitangaza kuwa ni label ya kusaidia wasanii kwa kuwa msaada wanaoutoa ni wa kawaida na sio wakutangaza mitandao.
Hata hivyo Joh hakusita kuelezea mahusiano ya weusi na Lord Eyez
“Lord hajatengwa na bado ni mmoja wa wanafamilia katika kundi letu la Weusi, kuna wimbo wa Lord tulikuwa studio tukiuandaa juzi japo watu wanaongea mengi kuhusu ukaribu wetu na Lord kwa sasa ila siyo mbaya wakituzungumzia kwa kuwa ni sehemu ya maisha yetu”alisema Joh.

Mwana FA huenda akaachia ngoma mbili kwa mpigo, ikiwemo remix ya Asanteni kwa kuja (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Kwa muda mrefu, Mwana FA amekuwa akizungumzia kuja na remix ya wimbo wake, Asanteni kwa Kuja.
Hivi karibuni alidai kuwa ni mtu mmoja tu aliyekuwa hajamalizia kuingiza verse yake lakini wote aliowashirikisha wamekamilisha.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, rapper huyo amewauliza mashabiki wake kama wanataka aachie remix hiyo au atoe ngoma nyingine.
Mashabiki wamekuwa na mtazamo tofauti lakini kuna uwezekano akaja kutoa ngoma zote mbili. Ni kwasababu mkali huyo amemaliza kushoot video ya wimbo wake mpya nchini Afrika Kusini.