Saturday, April 29, 2017

Jux akanusha tetesi za Kuachana na Vanessa Mdee(WWW.BABALAOINK.BLOGSPOT.COM)

SIku chache zilizopita zilizuka tetesi kwamba mastaa wawili wa muziki ambao wako katika mahusiano ya kimapenzi, Vanessa Mdee na Jux wameachana.
Tetesi ambazo zilizua gumzo katika mitandao ya kijamii, ikiwa hatukupata kauli yoyote kutoka kwa wahusika hao wawili.
Kwenye XXL ya Clouds FM Jux alikuwepo kutambulisha ngoma yake mpya ambayo ameipa jina la Umenikamata, na moja kati ya maswali ambayo aliulizwa ni kuhusu tetesi za kuvunjika kwa mahusiano yake na Vanessa.
Jux amekanusha tetesi hizo na kudai kwamba wao wako vizuri, ila tu ni tetesi ambazo zimezuka baada ya kutoonekana kuwa karibu na Vanessa kwa muda sasa.

Alichokisema Fid Q kuhusu Sakata la Bongo Movie na Movie za Kigeni (WWW.BABALAOINK.BLOGSPOT.COM)

Moja kati ya habari kubwa sana ambazo zinatrend kwasasa Bongo Tanzania ni pamoja na sakata la kuzuiwa kwa movie za nje ambazo zinatafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili ambazo zinadaiwa kuharibu soko la filamu za ndani.
Mengi tumeyasikia na wengi wameongea, ila mkali wa Hiphop Tanzania Fareed Kubanda almaaruf kama Fid Q naye alikuwa na yakwake ya kusema kupitia kipindi cha leo Tena cha Clouds FM hapo jana.
Fid Q amepongeza harakati ambazo zinafanywa na mastaa wa Bongo Movie na kudai kwamba wanahitaji kusapotiwa juu ya hilo na pia akawapa ushauri mdogo ambao yeye anahisi unaweza kuwa msaada kwao.
Kimoja kati ya vingi ambavyo Fid Q amewashauri Bongo Movie, ni kujipanga na kuwa kama team moja na kutoa kazi zao kwa mpangilio ili kuzi-push kazi hizo na kuhakikisha zinafika mbali tofauti na kuwa kwa wiki wanatoa filamu 5 au 10.

Wednesday, April 26, 2017

beat ya ‘Humble’ ya Kendrick Lamar ilikuwa kwa ajili ya rapper huyu(WWW.BABALAOINK.BLOGSPOT.COM)

Ikiwa bado inakimbiza chati za Billboard kwa kuingiza nyimbo zote 14 kutoka kwenye album yake ya “Damn”. ngoma ya Humble ya Kendrick Lamar beat lake lilikuwa kwa ajili ya Gucci Mane.
Baada ya “Humble” kujitengenezea rekodi kwa kumtoa Ed Sheeran kwenye chati za Billboard, producer Mike Will Made it amefunguka kwa kusema kwamba mdundo wa ngoma ya “Humble” ambao ameutengeneza, OG yake ilikuwa ni kwa ajili ya Gucci Mane pindi atakapo toka jela basi mdundo huu ungetumika kumfanya kusikika zaidi redioni, ila mambo yakawa si mambo kutokana na Mike Will Made It kushindwa kumpata Gucci ndipo akaidondosha kwa Kendrick Lamar na akafanikiwa kuileta “Humble” ambayo inaumiza kwa sasa.
Mike Will Made It aliendelea kufunguka kwa kusema kwamba Beat hiyo ilikuwa na swag flani hivi za kundi la NWA ambapo unaweza kufeel kama midundo kutoka kwa Eminem au Dr Dre.








With “HUMBLE.,” I knew that beat was going to capture a moment. It just felt real urgent. I made that beat [last year] when Gucci Mane was getting out of jail; I made it with him in mind. I was just thinking, damn, Gucci’s about to come home; it’s got to be something urgent that’s just going to take over the radio. And I felt like that beat was that. I ended up not doing it with Gucci and I let Kendrick hear it. I was thinking, if Dot gets on this it’ll be his first time being heard on some[thing] like this. At the same time, it kind of has an NWA/Dr. Dre feel, an Eminem kind of feel. So I thought, let me see if Dot f**** with it. And he heard the beat and he liked it. But he was about to give me “HUMBLE.” for [my album] Ransom 2. I love that song so I was like, ‘Man, hell yeah.’ Then he told me that his team was saying he should keep it. And I told him, ‘Bruh, you definitely should keep it, and you should use it as your single.'”

Thursday, April 6, 2017

C.E.O WA TONGWE RECORD AONGEA KUHUSU YALIOMPATA ROMA NA MONI CENTROZONE [WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM]

 
TAZAMA VIDEO https://youtu.be/83invTQLMSs  IKIMUONYESHA C.E.O WA TONGWE RECORD J MURDER AKIONGELEA KUKAMATWA KWA ROMA NA MONI

NEW VIDEO |POCHI| WATU WABAYA & ROTTEN BLOOD |[WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM]

NEW VIDEO #POCHI .BOFYA https://m.youtube.com/watch?feature=youtu.be&v=6pd7YVkrlKQ Kutizama Video mpya #Pochi Directed by Nicklass ..Produced by BIN LADEN ,Mixed by Davy Machords & Ttouchez ..#HAPOKWENYEPOCHIIII

Tweets za Zitto Kabwe, Vanessa Mdee kuhusu Kukamatwa Roma & Moni Central Zone [WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM]

Kuanzia usiku wa jana kumekuwa na taarifa ambazo sio nzuri kuwahusu wakali wawili wa muziki hapa Bongo Roma Mkatoliki na Moni Centralzone kukamatwa na watu wasiojulikana na kupelekwa sehemu ambayo mpaka sasa haijafahamika.
Taarifa hizo zilianza kwa Mbunge wa Mikumi Mh Joseph Haule (Professor Jay) kwa kuposti taarifa hiyo kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Taarifa hiyo imewagusa wengi hasa watu maarufu na kila mmoja ameweza kuandika yakwake, ila kwasasa nimekusogezea tweets za Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Zuberi Kabwe na Vanessa Mdee.

Uvamizi wa studio ya Tongwe na kumkamata msanii Roma Mkatoliki ni mwendelezo wa uongozi wa kigangstar na lazima kulaani Kwa nguvu zetu zote

                                                    VeeMoney #CashMadame @VanessaMdee
Roma na Moni wamerudishwa? Maana nililala nikadhani labda ndoto mbaya tu hii.

Sony Music yamsaini msanii mwingine wa Nigeria baada ya Davido na WizKid [WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM]

Ni nadra sana kukuta msanii wa Afrika anafikiriwa kuwa kipaumbele kwa lebo yoyote kubwa ya kimataifa hasa kama Sony Music, lakini kwa nyuzi kali za Tekno ni wazi kuwa wasanii kutoka Afrika wamekuwa wagumu kuwapotezea.
Mtandao wa Billboard umethibitisha taarifa zilizokuwa zinasambaa juu ya Sony Music kutaka kumsignisha Tekno kwenye lebo yao. Kwa mujibu wa taarifa iliyoandikwa kwenye mtandao huo, staa huyo wa muziki kutoka Nigeria amesign mkataba mnono wenye thamani ya USD 4 Million na Colmbia Records kampuni inayomilikiwa na Sony Music.
Tekno
Vice President na A&R wa Colombia Records Imran Majid aliiambia Billboard kuwa, Tulivutiwa na Tekno baada ya kuusikia Pana ukisikilizwa na watu wengi Marekani, Uingereza na Canada, ila binafsi nilikutana na wimbo huo baada ya kuona video iliyokuwa iki-trend Facebook ya wapenzi wakiucheza wimbo huo beach. Niliusikiliza mara mbili mbili, nikaupenda, nikawaambia na watu wangu ofisini….”
 Aliongeza Imran Majid,Kuna wasanii wengi wazuri wanaibuka kutoka West Africa, na muziki wao unakuja kwa kasi kubwa na kusikilizwa sana na watu Marekani, Uiingereza, Canada na karibia Ulaya nzima”.
Mkataba wa msanii huyo upo tofauti kidogo na mikataba waliosign Wizkid na Davido, mkataba wa Tekno na Colombia Records ni wa kurekodi nyimbo tatu zitakazo simamiwa na Colombia Records, SONY Music na kusambazwa kwenye soko la kimataifa ikiwemo Marekani yenyewe, Uiingereza, Canada na sehemu nyingine duniani, lakini dili hilo haitomzuia Tekno kurekodi au kutoa nyimbo kwa mashabiki wake wa Africa.
“Tekno ana team ya watu wazuri na wanaomsimamia vizuri kwenye soko la muziki Africa, hivyo anaweza kuendelea kwa wakati wowote kurekodi au kuachia nyimbo kwa ajili ya watu wake wa nyumbani na Africa kwa ujumla, ila kwa upande wetu, sisi tutaweka nguvu nyingi zaidi kwenye kuusogeza wimbo wa Pana kwa wasikilizaji wengi zaidi wa huku” Majid aliiambia Billboard
 Kwa mujibu wa mtandao wa Pulse.ng wa Nigeria, single ya ‘Pana’ sasa ni mali rasmi ya SONY Music na Tekno atatakiwa kurekodi tena nyimbo nyingine mbili chini ya Colombia Records, nyimbo hizo zitazingatia vigezo vilivyo orodheshwa kwenye mkataba wao na perfornace ya nyimbo hizo ndio zitaweza kuishawishi lebo ya Colombia Records kuongeza mkataba wao na Tekno au kuishia tu na nyimbo walizokubaliana.
Source: Billboard/ Pulse.ng

UJIO MPYA WA B.O.B [WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM]

Baada ya kuwa kimya kidogo, B.O.B amerudi upya na ujio wa Album yake mpya ya  ETHER inayotarajiwa kuachiwa May 12 mwaka huu.
Album ya “EITHER” ndio itakuwa album yake ya kwanza baada ya mkataba na Grand Hustle/Atlantic Records kuisha na hiyo itakuwa Album yake ya nne tangu kuanza kuachia kazi zake, kupitia kurasa yake ya Instagram, B.O.B aliposti cover art ya Album yake hiyo ya “EITHER”.

Prof Jay: Nimestushwa!! Watu wavamia studio za Tongwe na kumteka Roma na Moni Central Zone

Mbunge wa Mikumi, Joseph Haule aka Professor Jay, amesema rapper Roma Mkatoliki pamoja na rapper Moni Central Zone wamechukuliwa na kupelekwa kusikojulikana na watu waliozivamia studio za Tongwe Records jana usiku.
Profesa amedai watu hao wamemchukua pia kijana wa kazi, computer ya studio pamoja na TV.
(Instagram post)
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Profesa alitoa taarifa hii.. “ROMA MKATOLIKI AMEKAMATWA USIKU HUU… Nimestushwa sana kusikia kuwa kuna watu wamevamia studio za TONGWE RECORDS majira ya saa moja usiku na wamemchukua ROMA @roma2030 , MONI @moni_centrozone na kijana wa Kazi na pia wamechukua COMPUTER ya studio na Screen (Tv) na wameondoka navyo kusikojulikana.. Mpaka sasa hatujui wamewapeleka wapi!!”

NEW AUDIO |LORD EYEZ HELA YANGU FT JUX| WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM

#BrandNewTzAudio 
LORD EYEZ ft JUX Bofya https://mkito.com/song/16272 
#HelaYanguNtaipataje produced by @kingluffa & @chizanbrain