Monday, October 31, 2016

Majibu ya Kala Jeremiah kuhusu remix ya “Wanandoto” na mashabiki.(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Takriban miezi miwili sasa imepita tangu msanii wa Hiphop Kala Jeremiah alipotoa ahadi ya kufanya remix ya wimbo wake wa “Wanandoto” na mashabiki zake wenye vipaji na kutoa tamko la kwamba mashabiki hao wawe wanajirekodi video fupi huku wakiimbia beat ya Wanandoto kwa kutumia mistari yao binafsi na kupost katika kurasa zao za instagram na kuweka hash tag ya Wanandoto (#Wanandoto).
 “Project ya wanandoto remix inaenda vizuri na washiriki wote 8 wamekwisha ingiza sauti, kutoka mikoa mbali mbali na mmoja kutoka Kenya. Imebaki tu sehemu yangu mimi kwasababu nina kama miezi miwili sipo Dar, niko mikoani kuna kazi fulani naifanya na hivyo mimi ndio nimekuwa kama kikwazo katika ucheleweshwaji wa hii project. Lakini all & all mwishoni mwa mwezi wa 11 narudi Dar es Salaam na kitu cha kwanza ni kwenda studio na kukamilisha hicho kitu na baada ya hapo process zingine zitafuata.”Asema Kala Jeremiah

Lord Eyes adai Ray C bado ana ‘chumba’ chake (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Rapa Lord Eyes ambaye ni mmoja wa wasanii wa kundi la Weusi amefunguka na kusema msanii Ray C bado ana chumba chake kwenye muziki na kusema yeye bado anamuombea kwani kwa matatizo aliyonayo kwani yale ni kama maradhi hivyo hayaponi kwa siku moja.
Lord Eyes ambaye kwa sasa amepumzishwa
kwenye kundi hilo, alisema hayo kupitia kipindi cha eNEWZ kinachorushwa na EATV na kusema kuwa mpaka sasa yeye hawasiliani wala kuongea na Ray C na kusema ila anamuombea Mungu apone na arudi kwenye muziki kama zamani kwani nafasi yake kwenye muziki bado ipo.
Ray C
“Leo hii kwenye muziki hatumuoni mtu kama Ray C, mpaka sasa hakuna mtu kama Ray C hivyo chumba chake kwenye muziki bado kipo kinamsubiri arudi tu.
Aliendelea “Sijakutana naye wala hatuongei ila namuombea Mungu kwani tatizo lile ni kama maradhi mengine hivyo haliwezi kuisha kwa mara moja linachukua muda, anahitaji maombezi na mimi namuombea kama navyojiombea mimi nifanye kazi zikamilike tukutane kwenye show huko” alisema Lord Eyes

Mr. Blue afunguka inshu ya kutopata tuzo tangu aanze muziki (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Msanii wa Bongo Fleva nchini Mr. Blue ameweka bayana kwamba pamoja na kukubalika na mashabiki wengi na kuwa kwenye tasnia ya muziki kwa muda mrefu hajawahi kupata tuzo hata moja ya kutambua mchango wake kwenye muziki.Mr Blue
Akizungumza katika kipindi cha Friday Night Live (FNL) kinachorushwa na EATV, Mr. Blue amesema anatambua umuhimu wa msanii kupata tuzo ila kwa bahati mbaya yeye hajawahi kupata tuzo.
“Mimi sijawahi kupata tuzo yoyote siyo ya kitaifa wala ya kimataifa ila ninachoamini mimi ni kwamba mimi ni ‘expensive’ na ndiyo maana natoa ngoma mara moja kwa mwaka na inadumu kwa muda mrefu” Amesema Mr. Blue
Aidha Mr. Blue ameongeza kuwa tuzo ambazo
zimeanzishwa na kituo hicho zitasaidia sana wasanii wengi kuweza kutambulika zaidi na anaamini pengine anaweza kupata tuzo hiyo na ikawa tuzo yake ya mara ya kwanza.

Sunday, October 30, 2016

Bifu la The Game na Meek Mill bado lipo, Meneja wa The Game athibitisha (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Baada ya Rick Ross kutangaza kuwa bifu la The Game na Meek Mill limeisha, Meneja wa The Game anasema bado bifu lipo na hatua iliyofikia ni kupeana kipigo tu.
Hivi karibuni Rapper Rick Ross alifunguka kutumia kurasa yake ya Snapchat kwa kusema kwamba bifu la The Game na Meek Mill amelimaliza, ila jipya limeibuka kwa meneja wa The Game na kusema kwamba Bifu bado lipo pale pale.
Meneja wa The Game, Wack 100 alifunguka kwa kukoment katika video ambayo ilikuwa ikimwonyesha Rick Ross akiongea kwamba bifu la The Game na Meek Mill limeisha

Saturday, October 29, 2016

Alikiba na ujio mpya wa Abby Skillz (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Abby Skillz ni msanii mkongwe wa Bongo Fleva ambaye aliwahi kupata nafasi ya kuhit na ngoma zake kadhaa kipindi cha nyuma.
Kimya cha muda mrefu ndio jini ambalo lilimkumba Abby Skillz na kujikuta akipoteza kabisa nafasi yake katika game ya music kutokana na muziki kubadilika na wasanii wakali kuongezeka kila iitwayo siku.
Kutokana na makubwa ambayo aliwahi kuyafanya Abby Skillz wakongwe wenzake Mr Blue pamoja na Alikiba hawakusita kumshika mkono na kumpa msaada ili kuhakikisha mkali huyo anarudi katika ramani ya music na anasimama imara kama ilivyokuwa zamani kutokana na kuamini kwenye uwezo wake. Ndipo walipoamua kukaa chini na kutengeneza ngoma ambayo wameipa jina la Averina.
Jana wakali hao watatu walikuwa katika media tour kituo cha Clouds Fm katika kipindi cha Leo Tena, ndipo Alikiba alizungumza haya kuhusu ujio mpya wa mkali huyo.
“Muziki umechange lakini kuna wasanii wakongwe ambao hawajui kama muziki umebadilika, wasanii wakongwe kama kina Abby Skillz wapo wengi, na wengi wameshajaribu kurudi tena lakini wanashindwa kufika zile levels ambazo watu wanazitaka sasa hivi, yote ni kwasababu hawajagundua ni kitu gani ambacho sasa hivi kinaendelea. Wanachotakiwa ni kusoma alama za nyakati kisha wasanii ambao wapo katika game wasiache kutoa sapoti kama mimi na Mr Blue tulivyotoa sapoti kwa Abby Skillz.”
Hayo ni machache tu kati ya mengi ambayo yamezungumzwa na Alikiba.

Dj khaled ameshare sehemu ya kwanza ya kitabu chake “The Keys” (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Dj khaled ameamua kushare sura ya kwanza ya kitabu chake cha “The Keys”
Baada ya kutangaza kuwa kutakuwa na ujio wa kitabu chake kipya cha “The Keys” ambacho kinatarajiwa kutoka Novemba 22, jana Octoba 28, Khaled alishare sehemu ya kwanza ya kitabu chake kwa mashabiki zake.
Sehemu ya kwanza ya kitabu hicho kimepewa jina “Stay Away from They”, katika sehemu hiyo ya kwanza anapoongelea “Stay Away from They” anaamanisha kwamba kwa mtu ambaye unahitaji kuwa na mafanikio basi jaribu kuwa mbali na ambao wanakurudisha nyuma katika mambo yako ya mafanikio, hii inamaanisha kuchagua marafiki ambao ni sahihi kwako.
“YOU’RE GOING TO BE SO MUCH BETTER ONCE YOU STAY AWAY FROM “THEY YOU’LL FEEL LIKE YOU’RE LIVING A WHOLE NEW LIFE, A LIFE FREE OF HATE, DOUBT, ENVY, AND TRASH VIBES, AND LET ME BE THE ONE TO TELL YOU THAT THAT’S WHEN YOU CAN START WINNING. MAJOR KEY: THE UNGRATEFUL AND JEALOUS “THEY”S ARE THE MOST DANGEROUS “THEY”S OUT THERE.”

Friday, October 28, 2016

New Audio: Ben Boyce ft Country Boy - Mjini Mipango(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Artist: Ben Boyce ft Country Boy
Song: Mjini Mipango
Contact:
Boyce: +255 625 573389 / +255 677 271492
Bofya hapa kusikiliza https://www.hulkshare.com/7mta0x5xj05c
#InfoPowered by @babalaotv @rodgersbabalao27 www.babalaoinc.blogspot.com
+255756978662
+255714010913 

New Audio: Miracle ft. Simao - Hakuna Matata (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Artist: MIRACLE FT SIMAO
Song: HAKUNA MATATA 
Producer: GOEFF MASTER Studio: TONGWE RECORD
Contact: 
Simao:  +255658299041
Miracle: +255653408028
Bofya hapa kusikiliza https://www.hulkshare.com/y3c8l8osf0g0
+255756978662

New Audio: Zipporah ft. Miracle - Nimechoka (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Artist: ZIPPORAH FT. MIRACLE
Artist Contact: +255 766 348 297
Producer: BELLO BIN LADEN
Studio: BIORN PRODUCTION
Bofya hapa kusikiliza  https://www.hulkshare.com/ajkewhfygi68
#InfoPowered by @babalaotv @rodgersbabalao27 www.babalaoinc.blogspot.com
+255756978662
+255714010913

NEW AUDIO: King Sumbali - Tupate Flavour(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Artist:   King Sumbali
Song:   Tupate Flavour
Producer: Dash Touches
Artist Contact: +255653819846
Bofya hapa kusikiliza  https://www.hulkshare.com/5tyyrsvcefsw#InfoPowered by @babalaotv @rodgersbabalao27 www.babalaoinc.blogspot.com

Wednesday, October 19, 2016

CHURA WA SNURA ANAPOKUTANA NA CHURA WA WITNESS KIBONGE MWEPESI (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Bofya hapa https://youtu.be/Z_q_frMEWIU  kutazama official video ya WITNESZ KIBONGE MWEPEC OCHU SHEGGY ft SNURA MZEE YUSUPH
InfoPowered by @babalaotv @rodgersbabalao27 www.babalaoinc.blogspot.com
+255756978662
+255714010913 

MAGA V KILO..OFFICIAL VIDEO (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

New Video:KILO
Artist:MAGA V
Bofya hapa https://youtu.be/i4RlJez9-kY kutazama kilo ya Maga V kutoka KALI GANG
InfoPowered by @babalaotv @rodgersbabalao27 www.babalaoinc.blogspot.com
+255756978662
+255714010913

NEW AUDIO: TEA SIGWER - NYOTA NDOGO (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COOM)

Artist Name: Tea Sigwer
Song: Nyota Ndogo
Producer: Cat P
Studio: El Nino Music
Artist Contact: +255 678 992264
Bofya hapa https://www.hulkshare.com/rfd7ircvl7uo kupakua wimbo wa TEA SIGWER 
InfoPowered by @babalaotv @rodgersbabalao27 www.babalaoinc.blogspot.com
+255756978662
+255714010913 

NEW AUDIO: MSABILa - USIUWEKE (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Artist: MSABILA
Song: USIUWEKE
Studio: JJ RECORDS
Artist Cont: +255 653 528 666
Bofya hapa https://www.hulkshare.com/21e6cihqjq6o kupakua wimbo wa Msabila 
InfoPowered by @babalaotv @rodgersbabalao27 www.babalaoinc.blogspot.com
+255756978662
+255714010913 

Thursday, October 13, 2016

CHAKI BILA UBAO (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

CHAKI BILA UBAO

Zimepita siku miezi sasa miaka,
Chaki ilotoweka wengine twaisaka,
Uadilifu pasi na mashaka,
Ubaoni kwetu umefutika,
Chaki bila ubao Mwalimu twakulilia.

Ulianza na Tanu tamaa hukuikata,
Bila kumwaga damu ukawapa mchakamchaka,
Chama shika hatamu ukawatoa vibaraka,
Leo mambo matamu hakika twakukumbuka
Chaki bila ubao Mwalimu twakulilia.

Tukapata na uhuru bendera ikapepea,
Mengi twashukuru japo machache tumepelea
Rasilimali kila kona ulizitunza
Utajiri wetu ulionona haukuuchuuza
Ulituhimiza kusoma tuje faidi vilivyonona
Chaki bila ubao Mwalimu twakulilia

Siwezi maliza,kuandika nitosheke
Waliopo ntawajuza, wasome wasibweteke
Nitakuja Musoma hadi Mwitongo nitokeze,
Ulipolala nifike, nyumba yako niishike
Chaki bila ubao Mwalimu twakulilia.


©Mgosi Mkoloni
APC (Arusha poetry Club) 

 marikifredy@gmail.com

#InfoPowered by @babalaotv @rodgersbabalao27 www.babalaoinc.blogspot.com
#APC

Wednesday, October 12, 2016

CHABA ANALOGA LYRICS (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Song;- #Analoga
Artists;- @chaba009 @hisiatz
Producer;- @daznaledge
Director;- @innomafuru

Intro;-
Mmmh! Tumeirudisha nyumbani, twende ss, haah×6 bounce! Haah×6 haya ss,
Bridge×2
Embu loga loga nikubambe mamii, embu loga nikubambe (loga, loga)
Verse1
Ayo kimwali huhitaji marashi,
Pamba kali uonekane mtashi,
Bila wanja una mvuto, Kifua chako hakiihitaji vito, Hivyo ulivyo ni vipodozi tosha,
Huhitaji poda ukanikosha, Mrembo unahitaji tuu kuoga,
Umbo lako ni shida linavyologa,
Japo umetoga, Hereni huhitaji,
Unaonekana una kipaji, Cha kuloga na mapozi na wako mwendo, Sauti yako inaniloga matendo, Tafadhali, nitake radhi kimwali, Unaloga mpaka nimehisi kuparty hatari unavyologa mabusu, Kukupapasa natamani uniruhusu, Unavyologa utamu kunoga, Mashiko manono kama maboga,
Nipo Arusha ila najihisi ulaya ulaya, Loga chochea more fire,
Bridge×2
Chorus×1
Natakaa unikaribiee, Uwe karibu namii, Nikugusee nikukunee, Nikupe rahaa,
Utabaki hoii hoii hoii mmh mmh! (Hoii, hoii)
Utabaki hoii hoii hoii mmh mmh! (Hoii hoii)
Verse2
Ayo subiri nikupe tahadhari, Huyu kimwali alivyo hatari,
Vile alivyo mahaba, Na umbile haba jamaa hulogeka na kumuhonga laga, Na dinner,
Akitaja jina analoga mpaka anahongwa carina, Mauno milogo mpaka amehongwa nyumba, Akafunguliwa account mavumba bila kwenda Sumba-wanga au Tanga hahitaji waganga mpe moja kanga,
Iwe kavu au ndembe, Kifuani maembe, Dodo yanavyologa, Utakoma soga, Analoga na misosi maridadi iwe mbuzi ama samaki na zake saladi hainiishi midadi, Tabia ka mlami, Analoga mahaba kama jini yaani,
Bridge×2
Chorus×1

Bonyeza link ya mkito hapo chini  kudownload audio
& Pls, listen & share Good music,

http://bit.ly/Analoga

#TanzaniteMilele

#InfoPowered by @babalaotv @rodgersbabalao27 www.babalaoinc.blogspot.com 

Selementally ft mabeste (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Bofya hapa https://www.hulkshare.com/21e6cihqjq6o 
kupakua wimbo wa Selementally ft mabeste uitwao Atanivunja shingo produced by j willz Studio MCB
#InfoPowered by @babalaotv @rodgersbabalao27 www.babalaoinc.blogspot.com

RICO SINGLE #Yaani Raha (WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Bofya hapa https://www.hulkshare.com/hyegij85axhc
 
Single:Yaani Raha
Artist: Rico single
Prods by Aloneym
Studio Islands rec Zanzibar
#keepsupporting
#keepsupporting
#InfoPowered by @babalaotv @rodgersbongohot27 www.babalaoinc.blogspot.com