Thursday, June 22, 2017

[NEW VIDEO] DIAMOND -I MISS YOU- [WWW.BABALAOINK.BLOGSPOT.COM]

Watch here https://youtu.be/P_bBv0cJLCg This Song was written by Diamond Platnumz & The beat was produced by LIZER CLASSIC from Tanzania from Wasafi Records Tanzania... The Video was shot in Johannesburg, South Africa by NIC

NEW VIDEO[DIAMOND FT TIWA SAVAGE -FIRE- [WWW.BABALAOINK.BLOGSPOT.COM]

Watch here https://youtu.be/ue5TNcJ3iRU This Song was written by Diamond Platnumz & The beat was produced by LIZER CLASSIC from Tanzania from Wasafi Records Tanzania... The Video was shot in Johannesburg, South Africa by NIC

Thursday, June 8, 2017

MSANII KUTOKA AFRIKA AKABIDHIWA JUKWAA KUELEKEA TUZO ZA BET [WWW.BABALAOINK.BLOGSPOT.COM]

BET wametoa orodha ya wasanii ambao watapanda katika steji ya utoaji tuzo usiku wa June 25 Jumapili mwaka 2017.
Tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika katika jiji la (L.A)Los Angeles nchini Marekani katika ukumbi wa Microsoft Theater , Hata hivyo msanii tokea bara la Afrika Wizkid nae ametajwa katika watu watakao weza kushiriki kutoa burudani kwenye Tuzo hizo kubwa huku list hiyo ikiwa na wasanii nguli kama vile Snoop Dogg, Wiz Khalifa, Pusha T, Desiigner, Bryson Tiller, Rae Sremmurd, Jhené Aiko na New Edition.
Katika awamu ya kwanza BET wamewataja pia wasanii kama Migos, Bruno Mars, Future, Trey Songz na Tamar Braxton ndio watakaoanza kupanda kwenye stage kutoa burudani katika usiku huo.
Tamasha hilo litakalo fanyika siku nne mfululizo litaoneshwa mubashara kuanzia saa mbili usiku.Msanii Beyonce na Bruno Mars ndio walio ongoza kutajwa katika vipengele tofauti, Huku Beyone akiwania vipengele saba, na Bruno Mars akiwania vipengele vitano.
Pia wasanii kama Solange, Chance the Rapper na Migos,wakiwa katika vipengele vinne vinne.

Hizi ndizo lebo anazozitamani Harmonize kufanya nazo kazi endapo akitemwa WCB [WWW.BABALAOINK.BLOGSPOT.COM]

Ukiizungumzia WCB unazungumzia moja kati ya lebo kubwa sana Barani Afrika, ikiwa Harmonize ndio mmoja kati ya wana wanaokinukisha katika lebo hiyo.
Harmonize amefunguka kuwa endapo kibarua kikiota nyasi kwenye lebo yake ya WCB zipo lebo ambazo yeye kama yeye anazitamani kufanya nazo kazi.
Harmonize amezitaja Young Money na Roc Nation kama ndio lebo ambazo anatamani kufanya nazo kazi akidai kwamba WCB ni lebo kubwa Africa kwahiyo endapo akiondoka hapo hatahitaji tena kurudi nyuma na hivyo ataenda worldwide.
“Ikitokea kufanya kazi na lebo nyingine, lebo yoyote tunaweza kufanya kazi ila me ninawish Roc Nation au Young Money kwasababu siwezi kutoka WCB nikaenda lebo nyingine ya kawaida kwasababu ukizungumzia WCB unazungumzia lebo kubwa Africa kwahiyo nikitoka Africa natamani kwenda worldwide.” Alisema Harmonize

Juma Nature anafeli kwasababu anakosa kampani yangu-: Mkubwa Fella [WWW.BABALAOINK.BLOGSPOT.COM]

Kama wewe ni shabiki wa Bongo fleva kuanzia miaka ya 2000 na kuendelea naamini utakuwa unalikumbuka kundi la muziki la TMK Wanaume, kundi ambalo lilikuwa likivikutanisha vichwa kama Juma Nature, Chege, Temba na hata KR MUllah.
Kundi ambalo baadaye lilikuja kugawanyika na kuibua makundi mawili ambayo ni TMK Wanaume Family na TMK Wanaume Halisi ambapo Juma Kassim Kiroboto ndiye ambaye alikuwa kiongozi wa TMK Halisi ambao walionekana kama kujiengua hivi katika umoja ule wa mwanzo.
Ni ukweli usiofichika kwamba hakukuwa na mafanikio makubwa kihivyo katika safari ya Juma Nature na wenzie kutokana na wengi wao kuwa wamepotea kwenye game kulinganisha na wasanii kama Chege na Temba ambao walibaki katika uongozi wa kundi na hadi leo wanazidi kutusua.
Mkubwa Fella ambaye ndiye alikuwa meneja wa kundi la TMK Wanaume enzi hizo na kutaka kuujua mtazamo wake juu ya kushuka kwa msanii Juma Nature kimuziki ukilinganisha na nafasi aliyokuwa nayo kipindi kile.
“Yule muziki wake haujapungukiwa, yule kapungukiwa kampani yangu, sababu muziki wake ndio uleule aliokuwa anafanya na muziki ni uleule, ila kampani. Kwasababu mimi ninaweza kuongea na mwenye radio vizuri, mimi naweza kuongea na Dj vizuri, yeye anaweza akatunga mashairi vizuri. Kikubwa unaweza kutunga mashairi vizuri lakini ukawa hauna kauli nzuri ya kuongea na Dj ama Mtangazaji lakini mimi naweza kuwa nayo busara hiyo, lakini sio kwamba nyimbo zake ni mbaya.” ALisema Mkubwa Fella.