Tuesday, November 8, 2016

Wale asakwa na polisi(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Rapper Wale amefunguliwa mashitaka na kampuni ya kuandaa matamasha baada ya kulipwa mtonyo wa dola $25,000 alafu hakutokea jukwaani.
Kupitia mtandao wa Tmz umeripoti kwamba rapper Wale amefunguliwa mashitaka na kampuni ya Upfront and Personal Global kwa kutotokea katika tamasha ambalo alipaswa kuperfome baada ya kupewa $25,000 ikiwa kama mkataba wao waliokubaliana.
Hata hivyo Promoter wa Tamasha hilo amefunguka kwamba walijaribu kumpigia simu Wale lakini alikuwa hapokei, promoter huyo anasema kwamba lengo kubwa la kumtafuta ni kutaka kurudishiwa pesa yao.

No comments:

Post a Comment