Thursday, February 2, 2017

Harmorapa amkosha P Funk kwa kitendo hiki(WWW.BABALAOINC.BLOGSPOT.COM)

Producer mkongwe na mwenye heshima yake P Funk Majani ameibuka na kumzungumzia huku akimsifia msanii anayeibukia kwa kasi katika bongo fleva, Harmorapa na kusema kuwa rapa huyo ni “level nyingine”.
Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na picha mbalimbali za Harmorapa mitandaoni zikimuonesha akiwa ameshikilia pesa nyingi jambo ambalo limemfanya producer huyo kuibuka na kumwagia misifa.
“Chezea Harmorapa wewe!!! Levo zingine hizi” alindika P Funk Majani kupitia ukurasa wake wa Instagram.
Tangu Msanii Harmorapa ameingia kwenye muziki kwa kuanza kujifafanisha na msanii Harmonize, kila wakati rapa huyo amekuwa akiingia kwenye ‘headline’ mbalimbali na kuzungumziwa na wasanii wengi wakubwa nchini, wengine wakifurahishwa na matendo yake huku wengine wakimdhihaki na kuona kuwa hastaili kuwa mwanamuziki.

No comments:

Post a Comment