Sehemu ya kwanza
______________________
Katikati mwa
Miaka ya 2000 kituo cha Luninga cha EATV ama Channel 5 kilikuwa na
kipindi kinachoitwa "In da House". Kipindi hicho kilikuwa hakina
mtangazaji maalumu ila kilikuwa na kawaida ya kumualika msanii ambaye
hugeuka mtangazaji na pia kuchagua nyimbo anazozipenda.
Kuna
kipindi alichaguliwa Kala Pina kuendesha kipindi hicho. Baada stori na
kuchagua nyimbo mbili tatu ikafikia wakati akaamua kumwambia VJ kwamba
ampigie wimbo wowote wa Immortal Technique. Kilichotokea ni kwamba yule
VJ hakucheza wimbo wa Immortal bali aliucheza wimbo wa Jay Moe
aliomshirikisha Mangwea uitwao "kimya kimya".
Nilichojifunza ni
kwamba kwenye hili game la Tanzania Jay Moe ni msanii pmaarufu kuliko
Immortal Technique. Pia Madj wengi wa sasa ni "waweka kanda" kama Vital
Maembe anawaita na sio wafuatiliaje wa muziki na ndio maana Vj
akashindwa kutofautisha kati ya Immortal Technique na Jay Moe nadhani
alidhani Kala Pina kasema Moe Technique ambayo pia ni "a.k.a" ya Jay
Moe.
Enewei, Juma Mchopanga au maarufu kwa jina la Jay
Moe ni mchanaji ambaye analijua hili game tangu hajaanza
kulicheza. Inaaminika ameanza kulicheza mwaka 1998 ikiwa ni
miaka ishirini tangu azaliwe mnamo tarehe 27/11/1978. Muziki huu
ambao umeanza kushika kasi mwanzoni mwa miaka ya 90 kuna
uwezekano mkubwa Jay Moe akiwa na miaka kumi na kitu akawa
analifuatilia game kwa ukaribu kwahiyo yupo sawa anaposema
analijua kabla hajaanza licheza.
Kuna taarifa zinaeleza
kuwa, Mwaka 1999 alianzisha kundi lililoitwa Underground Kingdom
na baadaye wakalibadilisha jina likaitwa Sewer Celibracy akiwa
na Jaffarai na Mchizi Mox. Mwaka 2000, Jay moe na kundi lake
walishiriki katika mashindano ya kutafuta vipaji yaliyoandaliwa
na Clouds Fm huko ndiko walikokutana na Mack 2 B, Lady Lou na
Solo Thang wakaunda kundi la Wateule baada ya kushinda na
kupata nafasi ya kurekodi album chini ya Bongo Records.
Jay
moe tangu ameanza gemu mwaka 98 mpaka leo yupo katika gemu
huku kukiwa hakuna dalili zozote za kusanda. Naamini hili hata
yeye alilijua mapema ndio maana akaamua kujibatiza jina la
Mbakiaji. Mashabiki ni mashahidi wazuri kwamba wengi wasanii
wamekuja wamemuacha na bado ngoma zake hazijachuja bado zinabamba
japo zina miaka kibao.
Jay moe yupo kwenye hili game
kabla Mamu hajaanza kugonga nakala za album. Mamu au kwa jina
maarufu kama mdosi chini ya kampuni yake iitwayo GMC wasanii
promoters Ltd iliyosajiliwa miaka tarehe 03/01/2001 (miaka mitatu
baada ya Jay moe kuanza game) na kupewa 40577 ni moja kati
ya kampuni za kwanza kwanza kuanza kusambaza kazi za wasanii wa
Tanzania.
Album ya kwanza ya Jay Moe iitwayo “Ulimwengu
ndiyo mama” iliyotoka mwaka 2002 ilisambazwa na GMC ikiwa na
vibao kama “Ulimwengu ndiyo mama”, “Mi Mshamba”, “Maisha ya
Boarding ft Dully sykes”, “Bishoo”, “Kama unataka demu”,
“Misosi, mitungi na pamba ft Ay”, “Mpenzi kwaheri”, “Safari
njema”, “Ulimwengu ndio mama rmx” na “Mvua na jua”.
“Mawazo ya Jay Moe” ni albamu yake ya pili iliyotoka mwaka
2005 na kusambazwa pia na wadosi pia (GMC) huku album yake ya
tatu “Mocumentary” haikuwahi kutoka japo ilitangazwa tangu mwaka
2007. Jay moe aliwahi kusema kwamba ameshindwa kutoa album
yake ya mocumentary kama alivyoahidi kutokana na kukosekana kwa
mwamko kwa wasanii kutoa album badala yake wamekuwa wakitoa
singo kwa sababu ya mabadiliko ya biashara ya muziki (Ayo,
2015)
Inawezekana pia album yake haikutoka kutokana na
msambazaji ambaye alimsambazia album yake ya kwanza na ya pili
kuachana na usambazaji wa nyimbo za muziki wa kizazi kipya.
Ruge (2013) aliwahi kusema “Gmc.. sasa hivi ni mwaka wao wa
pili na nusu hawajatoa hata album moja ya bongo flava
wanafikiri kwa mamu pamefungwa lakini mamu anaendelea na wasanii
wa Gospel na wanauza vile vile”.
Wakati Jay moe anatoa
album ya kwanza “Ulimwengu ndio mama” mwaka 2002 chini ya GMC
msanii mwenye album alikuwa anapokea Tsh 100 kwa kila tape
ambayo ilikuwa ikiuzwa 1,200. Pia katika album ya pili “Mawazo
ya Jay Moe” ya mwaka 2015 msanii mwenye album alikuwa akilipwa
Tsh 200 kwa kila kanda iliyokuwa ikiuzwa Shilingi 1500 (Dudubaya, 2010)
Itaendelea............
Imeandikwa na
Malle Hanzi
O715076444
©2016
Powered by @babalaoTV www.babalaoinc.blogspot.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
-
❝BABU MWENYE NYUMBA❞ {♡Love Story♡_____Part..19} ∪₥ri_____+ ℳtunzi: ₲eofrey Mustafa, ₳rtist Jafa ✍ ℳaahali: Dar es salaam🇹🇿 ₩ha...
-
❝BABU MWENYE NYUMBA❞ {♡Love Story♡_____Part..29} ∪₥ri_____+ ℳtunzi: ₲eofrey Mustafa, ₳rtist Jafa ✍ ℳaahali: Dar es salaam🇹🇿 ₩ha...
-
❝BABU MWENYE NYUMBA❞ {♡Love Story♡_____Part..26} ∪₥ri_____+ ℳtunzi: ₲eofrey Mustafa, ₳rtist Jafa ✍ ℳaahali: Dar es salaam🇹🇿 ₩h...
No comments:
Post a Comment