Msanii mkongwe katika muziki wa bongo
fleva, Juma Nature amembariki rapa anayechipukia Harmorapa na kuweza
kufanya naye kazi chini ya producer T Touchez, iliyopewa jina la ‘Kiboko ya Mabishoo’.
Katika kazi hiyo ambayo tayari imeanza
kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, Harmorapa amewachana baadhi ya
mastaa akiwemo dansa Mose Iyobo, na watu wengine ambao wamekuwa
wakim-‘diss’ kuwa hajui muziki na kusema yeye hajali maneno yao machafu
kwani yeye amekuja kutafuta pesa.
Mbali na Mose Iyobo Harmorapa amechana Jacquline Wolper, Aunty Ezekiel na watu wa WCB
Kwa mujibu wa Harmorapa anadai kuwa kwa
sasa wanafanya video ya kazi hiyo na kusema wanategemea video ya
ngoma hiyo kutoka siku za karibuni.
No comments:
Post a Comment